Burudani
“Tugawane Umaskini”
Juma Kassim Nature a.k.a Kibla anatarajia kuzindua album yake Ijumaa ya
tarehe 20 mwezi huu na anataka kuonyesha kuwa yeye ni mkali kwa kuvunja
rekodi ya kujaza ukumbi wa Diamond Jubilee katika uzinduzi huo.
“Naomba wapenzi wote wa Kibla waje wamuone Kibla yule wa zamani ambaye anakuja upya kabisa, watu walijuwa nimepotea lakini nataka kuwadhihirishia kuwa ni yule yule Juma Nature, waje kwa wingi” alisema Nature.
Hii itakuwa ni album ya nne kwa mwanamuziki huyo, album alizopata kuzindua ni kama Ubinadam Kazi, Histori na nyingine nyingi.
Album yake ya sasa inajulikana kwa jina la Tugawane Umasikini tayari iko sokoni.