Burudani

Proffesor Jay adai watu hawataki kuwatengeneza wasanii wa Tanzania kwa kuogopa dharau

Msanii mkongwe wa muziki wa Hip Hop Joseph Haule (Proffesor) amefunguka kwa kudai kuwa kuna baadhi ya watu hawataki kutengeneza kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa Tanzania kwa kuogopa kudharauliwa.
profesa Jay
Profesa Jay
Akizungumza na The cruise ya East Africa Radio,Proffesor Jay amesema ,wasanii wengi wanashindwa kufanya zitu vizuri kutokana na kukosa pesa, na watu ambao wanaweza kuwekeza kwenye muziki wao.

“Watu hawataki kuwatengeneza wasanii wa Tanzania ,mimi kuna siku nilishangaa jamaa mmoja hivi,bosi, bosi kwenye kampuni fulani hivi, akasema unajua wasanii wa Tanzania bwana ukiwatengeneza wakawa wakubwa wataleta dharau ,eti ndiyo sababu hiyo ,nikamshangaa huyu jamaa kaenda shule! ,mbona anaongea vitu viko negative ,Eti anaogopa kumuwekeza Proffesor Jay awe mkubwa kwasababu ya dharau,unajua bongo hapa hakuwa msanii mkubwa ,so wote tupotupo tu kwenye level hizi hizi,ukisema msanii mkubwa wa bongoflave hapa bongo ni nani?,muziki wa kizazi kipya hakuna,wote tumebaki tupo tupo kwenye level hizi hizi,kwaiyo hawataki tuondoke kwenye level hizi kwenda kwenye another level kwabababu wana wasiwasi tuta wadharau,tutakudharau vipi? Wakati umetuweka wewe na sisi tunaheshimu,Ohoh umetutengeneza sisi tangu zamani,sisi tumetengenezwa na watu wengine, mashabiki wametutengeneza ,media zimetutengeneza sasa tutakudharau vipi?,kwasababu kudharau ni hulka ya binadamu tu, yoyote unaweza ukamtengeneza na ata ukamweka chini lakini baadae anaweza akaku dharau”Alisema Proffesor Jay

Proffesor Jay amesema kuwa kuna baadhi ya wasanii wa nyumbani wasio wabunifu wamesababisha muziki wa kizazi kipya kwa sasa kuwa na ladha ya kinigeria.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents