Habari

Polisi atishia kumuua Michelle Obama


Afisa wa polisi wa jijini Washington D.C. anayehusika na kulinda maafisa wa ikulu ya White House nchini Marekani, amejikuta akipumzishwa kazi baada ya kudaiwa kutishia maisha ya First Lady, Michelle Obama.
Kwa mujibu wa gazeti la Washington Post, ofisa huyo anafanya kazi ya escort ya pikipiki na anadaiwa kusema kuwa angempiga risasi First Lady huyo.
Inasemekana aliwaonesha polisi wenzake picha ya bunduki ambayo angeitumia kumuulia.
Hata hivyo idara ya polisi ya jijini Washington imesema haina maelezo mengi kuhusiana na tukio lakini msemaji wake Gwendolyn Crump amesema kwenye maelezo:
“We received an allegation that inappropriate comments were made. We are currently investigating the nature of those comments.”
Idara hiyo pia iliwasiliana na ‘Secret Service’ kuhusiana na kitisho hicho.
Msemaji wa Secret Service Ed Donovan amesema mamlaka hiyo inalifahamu tukio hilo na inachukua hatua zinazotakiwa kwa uchunguzi maalum.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents