Burudani
Pink: Sitouza nyimbo zangu mtandaoni
Rapper wa kike, Pink ametangaza kutoa nyimbo zake bure mtandaoni, ili kuwapa fursa wapenzi wa muziki wake kuupata bila gharama.
Amedai kuwa ataanza kufanya hivyo muda muafaka ukifika kwakuwa anaamini bado muda huo kwake haujafika. Amesema anaamini kuwa anahitaji kujitangaza zaidi na kujipatika mashabiki wengi.
Pink ni mmoja wa wasanii wachache wa hip hop wanaofanya vizuri Bongo kwa sasa. Hadi sasa ameshatoa ngoma tatu zilizofanya vizuri zikiwemo Usiogope aliomshirikisha Young Dee, Music aliomshirikisha Mr Blue na Ngoma iliyotoka miezi miwili iliyopita.
Yupo chini ya Style Records za producer Mbezi.