Picha:Simba na Yanga watoka sare ya 1-1,baada ya vuta nikuvute
Mechi 26 za ligi kuu soka Tanzania bara msimu wa 2013/2014 imemalizika jana (jumamosi) kwa timu zote 14 kushuka uwanjani katika miji tofauti nchini,ambapo mchezo wa Yanga na Simba ulimalizika kwa kufungana 1-1.
Mchezaji wa Yanga Didier Kavumbagu (kulia) akijaribu kumotoka beki wa Simba
Yanga waliovuliwa ubingwa na Azam fc walikuwa wenyeji wa watani zao wa jadi, wekundu wa Msimbazi Simba sc kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Katika kipindi cha kwanza, Amiss Tambwe, Said Ndemla kwa nyakati tofauti walipata nafasi nzuri za kufunga lakini kukosa umakini kuliwanyima Simba mabao.
Winga wa timu ya Simba, Ramadhani Singano akiwa katikati ya mabeki wa Yanga
Yanga nao walifika mara kadhaa langoni mwa Simba, lakini Mrisho Ngassa na Didier Kavumbagu walishindwa kuzibadili nafasi hizo kuwa mabao.
Kipindi cha kwanza kilimazika kwa timu hizo kutofungana.
Kipindi cha pili, Yanga walitawala zaidi mchezo, lakini dakika 75 Haruna Chanongo aliifungia Simba bao la kuongoza.
Dakika ya 86 ya kipindi hicho, Saimon Msuva alichomoa bao hilo na mechi kumalizika kwa sare ya 1-1.
Kiungo mshambuliaji wa Simba, Haruna Chanongo alichezewa vibaya na mchezaji wa Yanga”
Mashabiki wa Simba wakifuatilia mchezo kwa makini
Mashabiki wa Yanga wakishangaa jambo
Mwigizaji wa filamu Mboto akisalimiana na shabiki wa Yanga
Shabiki akipewa huduma ya kwanza baada ya kuzimia
Shabiki wa Yanga akiwa amezimia
Wazungu wakijadili jambo huku wakifuatilia mchezo wa Yanga na Simba