Picha:Chege,Temba na Mkubwa na Wanawe watoa msaada hospitali Temeke
Chege, Temba, Aslay pamoja na kundi zima la Mkubwa na Wanawe Jumatano hii walitembelea katika wodi ya watoto ya hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam na kutoa misaada mbalimbali.
Said Fella akikabidhi msaada kwa wahusika wa hospitali hiyo
Akizungumza na waandishi wa habari Said Fela alisema wanajisikia vizuri kutoa msaada kama huo kwakuwa na wao ni wagonjwa wa baadaye.
“Tumeamua kuanza na watoto maana mimi ni mzazi na hata mke wangu anajifunguliaga hapa pia mimi nilikuwa mtoto na katika show yetu pengine wazazi waliopo hapa walipenda kufika lakini kutokana na kuuguza wakashindwa kufika. Na hii hatutofanya wilaya hii tu tukipata kingine kidogo basi tutapeleka na kwingine na hii isiwe sisi tumefunga milango wajitokeze na wengine kusaidia,” alisema.