Burudani

Picha: Zari The Bosslady na Diamond Platnumz ni Kimye wa Afrika!

Kabla ya kukutana na Diamond Platnumz, Zari the Bosslady alikuwa tayari ni mwanamke maarufu nchini Uganda.

10843996_788400007864260_370710352_n

Utajiri na urembo wake ulimfanya aitwe Kim Kardashian wa Uganda.

10865028_382562075238985_818972804_n

Zari anamiliki msululu wa magari ya kifahari yakiwemo Range Rovers, Bentley, Limousine, Mercedes Benz, Chrysler na mengine ambapo mengi kati yake yana plate number za jina lake.

10724877_1589323561304364_1899813225_n

Anamiliki mijengo kibao pamoja na biashara mbalimbali kikiwemo chuo kikubwa kilichopo nchini Afrika Kusini.

10895048_814572885250603_511527749_n

Kukutana na Diamond Platnumz ambaye ukubwa wake tunaufahamu, umemfanya msichana huyo mwenye watoto watatu kuwa na nguvu zaidi na ndio maana couple yao inaweza kufananishwa na ya Kanye West na Kim Kardashian.

10882008_615353935258291_1108907975_n

Kama ilivyo kwa Kimye, Zari na Diamond wana sumaku ya skendo.
Ni hivi juzi tu mkanda wa ngono wa Zari ulisambaa mtandaoni ambao uliisha kulikuza tu jina na umaarufu wake.

10898960_748284251916131_1688742375_n

Kwa sasa wawili hao wameanza kuongozana kama kumbikumbi. Baada ya kumsindikiza Diamond kwenye tuzo za Channel O kisha kuwa pamoja kwenye ‘Ciroc All White Party’ jijini Kampala, wawili hao wapo pamoja tena kwenye ziara ya Diamond ya Burundi na Rwanda.

10890825_964152936932883_307561565_n

Kwa ukubwa wao kila mmoja, wawili hawa sasa ni miongoni mwa couple zenye nguvu zaidi katika burudani barani Afrika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents