Picha: Wema Sepetu aachiwa kwa dhamana, Manji na Gwajima watinga polisi
Alhamisi hii malkia wa filamu nchini Wema Sepetu ameachiwa kwa dhamana ya shilingi milioni tano baada ya kupandishwa kizimbani kwenye mahamaka ya Kisutu jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka matatu yanayomkabili.
Wakati huo huo mfanyabiashara maarufu Yusuph Manji na askofu Josephat Gwajima wamewasili katika kituo cha kati cha polisi kwa ajili ya kutii agizo la mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paulo Makonda ambapo majina yao yalitajwa Jumatano hii kuwa miongoni mwa majina 65 katika orodha ya watu wanatuhumiwa kuhusika na madawa ya kulevya.
Tazama picha zaidi hapa chini.
Petit Man akimuongoza Wema kupanda gari baada ya kuachiwa kwa dhamana
Mwanasheria Albert Msando akiteta jambo na Wema ambaye yupo ndani ya gari
Mama Wema akiwa katika eneo la mahakama ya Kisutu kusikiliza kesi ya mwanae
Wafuasi wa Gwajima wakiwasili kituo cha kati cha polisi Dar es Salaam