Picha: Wasanii watakaotumbuiza kwenye Serengeti Fiesta Moshi waahidi makamuzi ya nguvu
Wasanii wanaotarajia kupanda katika jukwaa la Serengeti Fiesta 2014 Jumamosi hii mjini Moshi wameahidi show ya nguvu. Wenyeji wa mkoa wa Kilimanjaro, Mh Temba na Nay wa Mitego nao wamewaomba wakazi wa mkoa wao huo kwenda kwa wingi kwenye show hiyo.
“Unajua unapokuwa mwenyeji lazima uwape waliokuja kukusapoti burudani ambayo inastahili, kwahiyo hatutawaangusha ndugu zetu waje tu waone ndugu zao tutakachokifanya tunataka kufunika home, “walisema hayo wakati wakihojiwa kwenye kituo cha radio cha Moshi FM.
Wasanii wengine watakaokuwepo ni Recho,Chege,Dully Sykes,Feza Kessy, Alikiba,Maua Sama,Roma,Fid Q,Stamina,Shaa,Lamar na wengine.
Lamar
Shaa na Chege
Adam Mchomvu
Mapacha
Mh Temba atakuwa kiwanja cha home
Chege
Dully Sykes
Recho
Nay wa Mitego naye atakuwa home
Stamina
Roma Mkatoliki
Alikiba
Fid Q