Bongo Movie

Picha: Wasanii waosha magari kusaidia waathirika wa ajali za magari Muhimbili

Wasanii wa filamu wakiwemo Johari, Monalisa, Irene Uwoya, Odama, Richie pamoja na Jacob Stephan aka JB jana katika viwanja vya Biafra Kinondani jijini Dar es Salaam, wameendesha kampeni ya kuosha magari ili kuchangisha fedha itakayowasaidia waathirika wa ajali za barabarari waliolazwa kwenye wodi ya hospitali ya taifa ya Muhimbili.

Kajala Masanja akiosha gari
Kajala Masanja akiosha gari

Akizungumza na Bongo5 kwenye banda la Jaffary Carwash ambapo shughuli hiyo ilipokuwa ikifanyika, JB alisema kama wasanii wana wajibu wa kufanya shughuli za kijamii ili kuisaidia.

“Sisi kama wasanii tunaonyesha tunaweza kutumia nguvu zetu kuosha magari ili kupata pesa za kuwasaidia watu ambao wameathirika kwa ajali za gari. Kwahiyo hii ni sehemu ya wajibu wetu, tunawakaribisha watu waje waoshe magari yao,” alisema JB

JB akiwa na Irene Uwoyo
JB akiwa na Irene Uwoya

Richie na Kajala wakiwa na mteja wao baada ya kuosha gari lake
Richie na Kajala wakiwa na mteja wao baada ya kuosha gari lake

Johari na Monalisa wakiosha gari
Johari na Monalisa wakiosha gari

IMG_5483
Richie akiosha gari

Monalisa, Odama pamoja na Johari wakisubiria wateja
Monalisa, Odama pamoja na Johari wakisubiria wateja

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents