Picha: Wasanii wamtembelea Mzee Njenje, Tanga, azungumzia alivyopatwa na Kiharusi
Msanii mkongwe wa muziki nchini anayetambulika kwa kazi yake kupitia Kilimanjaro Band, Mzee Njenje anayesumbuliwa na ugonjwa wa kiharusi ametembelewa na wasanii mbalimbali wanaopanda Jumamosi kwenye Serengeti Fiesta 2014 mjini Tanzania na kuzungumza naye kuhusiana na afya yake pamoja na kupata nasaha zake.
Ali Kiba akiwa nyumbani kwa Mzee Njenje, Sahare Tanga
Akizungumza na waandishi leo akiwa nyumbani kwake maeneo ya Sahare Tanga Mzee Njenje amesema anashukuru Mungu kwakuwa sasa hivi anaendelea vizuri japo mwili hauna nguvu.
“Mimi nimepata stroke, sio kali kabisa lakini imeniathiri upande wa kushoto, mguu na mkono, sio mwili wote ni baadhi tu, ni mguu na mkono tu, sehemu ya kichwa iko safi,” amesema. “Hivi juzi nilikwenda nikafanya kukumbuka ya nyimbo zangu nikakumbuka nyimbo zangu kumi, ndio maana nikasema bado nipo strong ni mguu tu unaonisumbua unakuwa na ganzi. ”
Barnaba akizungumza na Mzee Njenje
“Nimeanza kuumwa tangu tarehe 9 December, tarehe ambayo nilienda kufanya show pale Escape, nilikuja nikaperform nikarudi nyumbani alfajiri nimeamka nikaenda chooni nikasikia mwili hauna nguvu,” ameongeza. “Lakini nashukuru sikuanguka, nilikaa kwenye kiti cha choo, wakanipeleka hospitali lakini baadaye nivyotoka hospitali wakaja jamaa kunifanyia massage. Hiyo ndio iliyoniumiza walitumia nguvu sana, kwahiyo wakawa wamenirudisha nyuma, lakini nashukuru kuna bimkubwa mmoja ndo ananisaidia sana. Mpaka sasa hivi bado nashindwa kujisaidia mwenyewe ingawa nazungumza vizuri.”
Baada ya kumjulia hali Mzee Njenje, wasanii walielekea kufanya interview katika kituo cha radio cha Breeze FM.
Tazama picha za matukio yote.
Linah, Blue pamoja na Mzee Njenje
Mr Blue
Mzee Njenje akizungumza kuhusu hali yake
Stamina akiwa na Young Killer nyumbani kwa Mzee Njenje
Vanessa akiwa nyumbani kwa Mzee Njenje
Wasanii mbalimbali wakielekea kumtakia hali Mzee Njenje