Picha: Wasanii wa bongofleva waibuka washindi katika mechi ya kuchangia waathirika wa tetemeko Kagera
Wasanii wa muziki wa bongofleva wameibuka washindi kwa penati tano kwa nne dhidi ya wasanii wa bongomovie katika mechi ya hisani kwa ajili ya kuwachangia waathirika wa tetemeko la ardhi Bukoba.
Wasanii wa bongofleva wakishangia ubingwa wao
Mechi hiyo ilimalizika kwa timu hizo kutoka sare ya moja moja, magoli yaliyopatika katika kipindi cha kwanza. Goli la wasanii wa bongo movie lilifungwa na Mteze na dakika chache baadae H.Baba aliweza kuisawazishia timu yake kwa goli la kichwa.
Katika mechi nyingine kati ya wabunge wa Yanga na wabunge wa Simba, wabunge wa Yanga waliondoka na ushindi baada ya kuwafunga wabunge wa Simba goli 5 kwa 2. Angalia picha za matukio mbalimbali.
Young Killer akisalimiana na Waziri, Nape
Wasanii wakishangilia goli
Washindi
Full shangwe
Tunda Man katika ubora wake
Baby Jay akiwa na mtu wake wa karibu
King Zilla
Mashabiki