Picha: Uzinduzi wa kipindi cha radio (igizo) cha ‘Shuga’ – Biafra Kinondoni
Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) kwa kushirikiana na na NICEF na kituo cha radio cha Clouds FM, leo kimezindua igizo la radio liitwalo ‘Shuga Radio. Uzinduzi huo umefanyika kwenye viwanja vya Biafra Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Wadau wakimsikiliza Kamishina wa Taifa wa TACAIDS Miss Faraja Kotta
Igizo hilo linawalenga vijana wa Tanzania likiwa na ujumbe kuhusu virusi vya HIV na Ukimwi.
Shuga lenye series 12 litakuwa likirushwa Clouds FM saa 8 mchana kila Alhamis na kupitia Kitulo FM iliyopo wilayani Makete, Njombe.
Shuga Radio inalenga kuwafanya vijana wajihusishe kwenye mazungumzo kuhusi HIV na Ukimwi kupitia burudani na elimu kuelezea tabia hatarishi za ngono katika jitihada za kupunguza maambukizi mapya miongoni mwao.
Mgeni rasmi kwenye uzinduzi huo alikuwa Mwenyekiti wa Dr. Fatma Mrisho aliyesema uzinduzi wa Shuga Radio ni wa muda muafaka na muhimu nchini kutokana na kuongezeka kwa maambukizi ya HIV.
Watu mbalimbali ambao walihudhuria uzinduzi wa kipindi cha Shuga ambacho kitaruka clouds Fm
Uzinduzi umefanyika
Faraja Kota na Mkurugenzi Mkuu wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga
Kamishina wa vijana wa Taifa wa TACAIDS
Msanii toka THT Mataluma akitumbuiza kwenye uzinduzi wa Shuga
Nancy Sumari akiongea jambo na Faraja Kotta baada ya uzinduzi wa kipindi cha Shuga
Nancy Sumari na Faraja Kota, katikati
Dances wa THT wakitoa show baada ya uzinduzi wa Kipindi cha Shuga