Habari

Picha: Ushahidi kesi ya malkia wa meno ya tembo waendelea Kisutu Dar

Kesi inayomkabili raia wa China, Yang Feng Glan (66) maarufu kama Malkia wa tembo imeendelea tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam ambapo Ijumaa hii ushahidi juu ya kesi hiyo ukiendelea kutolewa.

Malkia wa meno ya tembo akiingia mahakamani

Kesi hiyo inasikilizwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi chini ya wakili wa serikali Kishenyi Mutalemwa na wakili wa utetezi,Masumbuko Lamwai.

Mtuhumiwa huyo akiwa na wenzake wawili anatuhumiwa kwa kufanya biashara ya vipande vya meno ya tembo 706 vyenye uzito wa kg 18892 thamani yake ikiwa ni shilingi bilioni 5.4 bila leseni ya Mkurugenzi wa wanyama pori.

Kesi hiyo itasikilizwa tena machi 14/15 mwezi ujao. Angalia picha.


By: Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents