Habari
Picha: Ukuta wa stand ya Ubungo waanguka, wajeruhi watu 4 na kuharibu magari 24
Leo alfajiri ukuta wa stand ya mabasi yaendayo mikoani ya Ubungo jijini Dar es Salaam, umeanguka na kuzusha hofu kubwa kwa wasafiri.
Inadaiwa kuwa watu wane wamejerahiwa huku magari 24 yaliyokuwa yameegeshwa mahali hapo yakiharibika vibaya.Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Charles Kenyela alikuwepo kwenye eneo la tukio hilo ambapo alizungumza na waandishi wa habari.
Chanzo cha ajali hiyo ni mkandarasi aliyekuwa akibomoa ukuta huo bila kuchukua tahadhari. Hizi ni baadhi ya picha za tukio hilo kwa hisani ya mtandao wa Global Publishers.