Picha
Picha: Scotland kuendelea kuwa sehemu ya Uingereza, yaukataa uhuru
Scotland imepiga kura kuchagua kuendelea kuwa sehemu ya Uingereza baada ya wapiga kura wengi zaidi kuukataa uhuru.
Watu 1,914,187 wamepiga kura za ‘Hapana’ na kuwazidi 1,539,920 waliopiga kura za ‘Ndiyo’ sawa na 55% kwa 45%.
Kura zilizokuwa zikihitajika kupata ushindi ni 1,852,828. Waziri wa kwanza wa Scotland, Alex Salmond aliyekuwa akipigia debe kujitenga kwa nchi hiyo, amesema amekubali kushindwa.
Hizi ni baadhi ya picha za wananchi waliofurahia uamuzi huo.
Hizi ni baadhi ya picha za wale waliosononeshwa na uamuzi huo.