Burudani

Picha: Rais Kikwete amempa Wema Sepetu mchongo mnono?

Kushindwa kwake kwenye kura za maoni mkoani Singida hakumaanishi kuwa Wema Sepetu ameachana na masuala ya siasa.

11202984_1636037943276143_471862541_n

Ikiwa ni siku chache tu baada ya kupokea matusi ya kila aina kwenye Instagram baada ya kuwaita wale wanaoiunga mkono Ukawa ‘hawajielewi, Miss Tanzania huyo wa zamani anaonekana kupewa mchongo na Rais anayeondoka madarakani, Jakaya Kikwete.

11373988_436672513177263_1925022933_n
Rais Kikwete akisalimiana na waigizaji Wema Sepetu na Steve Nyerere

Haijajulikana wazi ni kitu gani Wema na Kikwete kimewakutanisha leo kwenye ikulu ya mjini Dodoma, lakini huenda kikawa ni kitu kitakachompa mkwanja wa maana mrembo huyo.. walau kutokana na kile alichoandika.

“Wakati nyie mnaongea upuuzi… Yangu yaninyookea….. Alhamdulillah… Wa moja havai mbili… Abadan asilan…. Earlier today… Ikulu… Dodoma… Thank u Mr.President,” ameandika Wema kwenye picha akiwa na Kikwete.

Si Wema tu atakayenufaika na mishe za uchaguzi mwaka huu.

11821713_860044667436328_1855019493_n

Wema amepost picha hiyo juu ya Steve Nyerere na kuandika:

Hongera sana ndugu yangu kwa kupewa nafasi hii kubwa… Nina imani hautotuangusha na yale tulioyapanga basi yatafanikiwa… Im so proud of you @stevenyerere2 … Haiya sasa twende tukatumikie jamii… Vijana wenzako tupo nyuma yako

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents