Habari
Picha: Rais Kenyatta wa Kenya amtembelea Rais mstaafu Daniel Arap Moi
Wakati Kenya ikiwa inajiandaa kwa Uchaguzi Mkuu, Rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta amemtembelea Rais wa zamani Daniel Arap Moi nyumbani kwake Kabarnet Gardens, Nairobi.
Kenyatta alimtembelea kumjulia hali Rais huyo wa zamani ambaye kwa sasa ana miaka 93. Daniel Arap Moi aliitawala Kenya kwenye awamu ya pili na kuiongoza kwa miaka 24 kuanzia 1979 hadi 2002.