Picha: Ommy Dimpoz asimulia alivyokutana na mrembo kwenye video yake mpya, afikiria kumleta kwenye uzinduzi
Ommy Dimpoz amesema kabla hata ya kufahamu kuwa Sofia Skvortsova ndiye model atakayemtumia kwenye video yake, alikuwa amemuona na akatamani msichana kama yeye aonekane kwenye video hiyo.
Ommy akiwa na Sofia Skvortsova
“Kwanza yule msichana wakati mimi natoka naelekea location, tupo kwenye taa hivi ambapo tunavuka taa ambazo ukizivuka unaelekea eneo la location nikawa namuona msichana yaani mzuri halafu nikawa nasema kimoyomoyo kwasababu nilikuwa sijamuona nikakutana naye location moja kwa moja, hatukukutana siku ya kwanza tukapanda, hapana, alikuja moja kwa moja siku ya kushoot,” Ommy ameiambia Bongo5.
Amesema baada ya kumuona Sofia alimwambia mshkaji wake kuwa anatamani msichana kama huyo awe kwenye video yake. Ameongeza kuwa siku ya kufanya video alipofika location akamkuta Sofia eneo hilo na kumchanganya zaidi Ommy.
“Baadaye Moe Musa ndio ananiita ananitambulisha ‘huyu ndio video model, sijui unamuonaje,” ameelezea Ommy. “Mimi nikamwambia, ‘mimi nimempenda sana’ mimi nilimuambia nataka msichana mzuri kulingana na uzuri wa nyimbo na maadhui ya nyimbo yalihitaji msichana mzuri.”
Ommy amesema kama mambo yakienda sawa anafikiria kumleta Sofia Tanzania siku ya uzinduzi wa video hiyo. Tangu amtambulishe kwenye Instagram, Sofia amepata followers wengi kutoka Tanzania. “Alipata followers wengi kutoka huku kwahiyo akashangaa sana halafu akaappreciate.”
Msikilize Ommy hapa:
Model huyo ni maarufu sana jijini London aitwaye Sofia Skvortsova. Sofia Skvortsova alizaliwa na kukulia Riga, Latvia. Ana asili ya Urusi, Ujerumani na Poland.
Kazi yake ya umodel hufanyia jijini London hufanya kazi na mawakala wa mamodel. Amekuwa akifanya shughuli hiyo kwa zaidi ya miaka mitano barani Ulaya na Mashariki ya Kati. Ameshaonekana kwenye majarida kibao, filamu, matangazo na video za muziki.
Mfahamu zaidi kwa picha hizi: