Burudani

Picha: Ni marafiki tu ama Jokate ameangukia kwenye penzi la muigizaji huyu wa Kenya?

Status ya uhusiano ya Jokate Mwegelo (kwa mujibu wake mwenyewe) inasomeka ‘single’ lakini huenda mambo yakawa yameshabadilika iwapo kile kilichopo katika mawazo yetu na yako baada ya kuona picha hizi kikawa ni kweli.

10499193_518296418302750_772355704_n
Nick Mutuma na Jokate Mwegelo

Mjenzi wa ufa uliokuwa umebomoka kwenye moyo wa Jokate kutokana na mahusiano yake yaliyopita (Hasheem Thabeet na Diamond), anaweza akawa ameshapatikana. Naye si mwingine ni muigizaji wa kipindi cha MTV Shuga na mtangazaji wa redio, Nick Mutuma.

Tangu aende Nairobi Kenya kikazi, Jokate na Mutuma wamekuwa karibu kiasi cha kuzalisha cheche za uwepo wa uhusiano kati yao. Kupitia Instagram, Mutuma alipost selfie akiwa na mrembo huyo aliyemlalia kifuani kama msichana afanyavyo kwa boyfriend wake.

Picha hiyo ilivuta macho na comments za wengi kwenye mtandao huo huku wengi wakisema wanapendeza kuwa pamoja.

“I pray u b a couple..those kids u’ll get tho’ lol @nickmutuma , @jokatem,” ameandika mmoja na mwingine kuchombeza: That is one cuuuute couple aaaaaaww!!!!

Jana pia Nick alipost picha hii ya TBT:

10454013_627658267333483_2040215902_n

Naye Jokate alipost picha ya Mutuma akiwa busy kwenye laptop na kuandika: #KenyanBoys always emoji @nickmutuma.”

10523536_260320557499404_699075074_n

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents