Picha: Mwili wa Nelson Mandela waagwa leo Pretoria
Asubuhi ya leo (December 11) mwili wa Nelson Mandela ulihamishwa kutoka mochwari ya hospitali ya jeshi na kupelekwa ‘Union Buildings’ katika mji kuu wa Afrika Kusini, Pretoria ambapo utakaa kwa siku tatu kwa ajili ya watu kuuaga kwa mara ya mwisho kabla ya mazishi yatakayofanyika weekend hii.
Jacob Zuma akitoa heshima zake
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini aliungana na wanafamilia wa Mandela mapema leo kutoa heshima za mwisho, akiwemo mjane mama Graca Machel, na mke wa zamani Winnie Madikizela Mandela pamoja na watoto wake.
Graca Michel
Viongozi wengine wa Afrika waliopata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwa Madiba leo ni pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete, Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe pamoja na watu maarufu wakiwemo mwanamitindo Naomi Campbell na Bono.
Robert Mugabe na mkewe wakienda kutoa heshima za mwisho
Gari iliyoubeba mwili wa Madiba
Baada ya viongozi watu wengine waliojipanga katika msululu mrefu walipata nafasi ya kumuaga Mandela aliyefariki dunia alhamisi iliyopita.
Mahali ulipolazwa mwili wa Madiba kwa ajili ya kuagwa ndipo sehemu alipoapishwa mwaka 1994 kama rais wa kwanza mweusi wa taifa hilo.
Mwili wa Mandela baadaye utapelekwa katika kijiji alichokulia Qunu kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika (December 15).
SOURCE: BBC, PICHA: REUTERS