Habari

Picha: Mwili wa Nelson Mandela waagwa leo Pretoria

Asubuhi ya leo (December 11) mwili wa Nelson Mandela ulihamishwa kutoka mochwari ya hospitali ya jeshi na kupelekwa ‘Union Buildings’ katika mji kuu wa Afrika Kusini, Pretoria ambapo utakaa kwa siku tatu kwa ajili ya watu kuuaga kwa mara ya mwisho kabla ya mazishi yatakayofanyika weekend hii.

South African President Jacob Zuma pays his respects at the coffin of former South African President Nelson Mandela, lying in state at the Union Buildings in Pretoria
Jacob Zuma akitoa heshima zake

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini aliungana na wanafamilia wa Mandela mapema leo kutoa heshima za mwisho, akiwemo mjane mama Graca Machel, na mke wa zamani Winnie Madikizela Mandela pamoja na watoto wake.

Graca Machel, the widow of former South African President Nelson Mandela, stands at his coffin as he lies in state at the Union Buildings in Pretoria
Graca Michel

Viongozi wengine wa Afrika waliopata nafasi ya kutoa heshima zao za mwisho kwa Madiba leo ni pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete, Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe pamoja na watu maarufu wakiwemo mwanamitindo Naomi Campbell na Bono.

Zimbabwe's President Robert Mugabe and his wife Grace hold hands as they walk away after paying their respects at the coffin of former South African President Nelson Mandela, which is lying in state, at the Union Buildings in Pretoria
Robert Mugabe na mkewe wakienda kutoa heshima za mwisho

The funeral cortege carrying the coffin of former South African President Mandela arrives at the Union Buildings in Pretoria
Gari iliyoubeba mwili wa Madiba

Cortege carrying the coffin of former South African President Nelson Mandela arrives at the Union Buildings, marking the start of a three-day lying-in state, in Pretoria

Military personnel carry the remains of the late Nelson Mandela upon arrival at the Union Buildings in Pretoria

Military personnel carry the remains of the late Nelson Mandela at the Union Buildings in Pretoria

Baada ya viongozi watu wengine waliojipanga katika msululu mrefu walipata nafasi ya kumuaga Mandela aliyefariki dunia alhamisi iliyopita.

Mahali ulipolazwa mwili wa Madiba kwa ajili ya kuagwa ndipo sehemu alipoapishwa mwaka 1994 kama rais wa kwanza mweusi wa taifa hilo.

Mwili wa Mandela baadaye utapelekwa katika kijiji alichokulia Qunu kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika (December 15).

SOURCE: BBC, PICHA: REUTERS

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents