Habari

Picha: Mvua zasababisha taharuki Dar

Siku ya jana ilionekana kuwa ngumu sana kwa wafanyabiashara na wasafiri kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha kusababisha kusimama kwa shughuli mbalimbali.

Mvua 3

Mvua iliyonyesha jana jijini Dar es Salaam imeonekana kuwa ni moja ya mvua iliyonyesha kwa muda mrefu tangu mwaka 2016 umeanza na kusababisha adha kubwa kwa wananchi wa jiji hili.

Mvua 2

April 26, Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ilitoa taarifa kwa umma juu ya uwepo wa mvua kubwa ambayo itaambatana na upepo mkali. Taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo iliyataja maeneo ambayo yataathirika ni pamoja na Dar es Salaam, Tanga, Pwani, Morogoro, Lindi, Mtwara na Visiwa vya Uguja na Pemba.

13102336_1572487909716665_257963960_n

Hata hivyo ripoti hiyo inasema kuwa mvua zitaendelea kuwepo mpaka kufikia Mei 9. Kutokana na utabiri huo wananchi wote tunaoishi kwenye mazingira hatarishi tunatakiwa kuchukua hatua zaidi kabla hatujapata madhara zaidi.

Mvua 1

Mvua hiyo iliyonyesha jana kwa takribani masaa kadhaa iliathiri miundo mbinu mbalimbali na kusababisha adha kubwa ya usafiri kwa wananchi, lakini pia mvua hizo zimesababisha nyumba kibao kujaa maji.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents