Burudani

Picha: Muonekano wa Zari The Bosslady baada ya kujifungua

Zari The Bosslady amerudi barabarani siku chache tu baada ya kujifungua mtoto wake wa pili na Diamond.

15306768_1860778600832845_7008999710648172544_n

Akiwa kwenye makazi mapya – kwenye nyumba yao na mchumba wake supastaa iliyopoto Pretoria, SA, mama huyo mwenye watoto watano kwa ujumla, hakutaka kuchelewa kurejea kwenye maisha yake ya kupendeza.

Amepost picha tatu Instagram ambapo ya kwanza akiwa kwenye gari ameandika: When mummy got some errands to run.”

15403295_181097955688339_5943800993211744256_n

Nyingine anayoonekana akiwa amempakata mtoto huyo wa kiume anayedaiwa kupewa jina ‘Riaz’ (kinyume cha jina Zari), ameandika: Simply do what suits your lifestyle and health in general.”

14504662_1810299332521752_5055692062381309952_n

Nyingine ameonekana akiwa amesimama kwenye mlango wa nyumba yao iliyonunuliwa kwa takriban shilingi milioni 400.

Pamoja na Riaz, Zari na Diamond ni wazazi wa mtoto maarufu zaidi kwenye Instagram barani Afrika, Tiffah.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents