Burudani
Picha: Mr Blue apata mtoto wa pili, jinsia yake ni?
Mr Blue na mke wake wamepata mtoto wa pili. Awamu hii familia hiyo imepata mtoto wa kike aitwaye, Khairriyaaa.
Khairriya Herry Sameer
“Alhamdulilahi mungu ni mwema sana sana, hatuna cha kumlipa zaidi ya kumuabudu kumtukuza na kumshukuru,” ameandika Blue kwenye Instagram.
“Nakushukuru sana mungu wangu na nakushukuru pia mke wangu @wahyda_bysers_heart kwa kuniletea zawadi nyingine nzuri. Nimepata mtoto mwingine wa kike ndugu zangu anaitwa# khairriyaaa…..ahsante mungu kwa kunipa baba na mama wa kunilea tena uzeeni.”