Picha: Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma anywa chai ya pamoja na wasanii wa Serengeti Fiesta
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma, Said Mwambungu aliwakaribisha wasanii ambao wanafanya show leo ya Serengeti Fiesta kunywa chai ya pamoja na na kuongea nao maneno machache.
Mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, ACP Mihayo Msekela
Mwambungu aliwasihi wasanii wapendane na kuwa kitu kimoja kwani umoja wao ndio utakaowasaidia katika kupambana na wizi wa kazi zao. Pia aliwakaribisha mkoano humo kufanya utalii wa ndani wajionee jinsi mkoa huo ulivyo na vivutio vyake mbalimbali.
Mkuu wa Mkoa, Said Mwambungu akiwaongoza wasanii kupata chai ya pamoja</strong
Kwenye chai hiyo alikuwepo pia mkuu wa wilaya ya Songea, Joseph Mkirikiti pamoja na Kamanda wa Polisi wa mkoa huo, ACP Mihayo Msekela. Wasanii hao waliambatana na Mkurugenzi wa Vipindi na Utayarishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba. Wasanii waliohudhuria ni pamoja na Madee,Linex,Recho,Barnaba,Mo Music,Baraka Da Prince,Godzilla,Mr Blue,TID, pamoja na watangazaji wa Clouds FM Shadee na Dj Fetty.
Ruge Mutahaba akiwatambulisha wasanii waliofika kwa mkuu wa mkoa wa Ruvuma
Said Mwambungu akiongea na wasanii
Mkuu wilaya ya Songea, Joseph Mkirikiti akiwakaribisha wasanii
Stamina,Godzilla,Recho na Madee wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma
Wakati wa kupata chai