Picha: Miss Lake Zone watoa msaada kwa watoto wa mtaani Mwanza
Washindi wa shindano la Miss Lake Zone lililofanyika jijini Mwanza mwishoni mwa mwezi uliopita, wamewatembelea watoto wanaoshi mtaani jijini Mwanza na kutoa misaada mbalimbali.
Mshindi wa pili wa shindano hilo, Mary Emanuel kutoka Shinyanga akiwapa vyakula na vinywaji watoto wa mtaani jijini Mwanza
Mshindi wa pili wa shindano hilo, Mary Emanuel kutoka Shinyanga, alijumuika na watoto hao kwa chakula na kuongea na wale wenye umri mkubwa na kuwaasa warudi kurudi kwao kuliko kuendelea kuishi katika mazingira hatarishi.
Mary Emanuel akiongea na watoto hao
Mshindi wa kwanza katika shindano hilo alikuwa mrembo wa Geita, Rachel Claver na mshindi wa tatu alikuwa ni Nicole Sarakyikya wa Shinyanga.
Shughuli hiyo iliandaliwa na waandaji wa shindano hilo, Flora Promotions chini ya taasisi yake ya ‘Nitetee Sauti ya Wanyonge’.
Washindi wa shindano la Miss Lake Zone lililofanyika Agosti 30 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza