Burudani
Picha: MC Pilipili afanya kile wachekeshaji wengi wa Bongo wanaogopa kufanya mikoani
Sio Alikiba na Diamond Platnumz tu waliojaza nyomi kwa show zao za sikukuu ya Christmas.
Wakati wakali hao na wasanii wengine wa muziki wakiingiza mamilioni ya shilingi jijini Dar es Salaam, mchekeshaji maarufu, MC Pilipili alikuwa na show ya kwanza ya komedi mjini Dodoma na kuvuta nyomi la kufanya mtu.
Sio kitu cha kawaida kwa mchekeshaji wa Tanzania kuvutia umati mkubwa wa watu mkoani, tena kwenye ukumbi maarufu kwaajili ya show ya komedi tu.
Kwenye wikiendi iliyopita, mchekeshaji huyo alizivunja mbavu za wakazi wa Dodoma kwa show yake kwenye ukumbi wa Royal Village. Hizi ni baadhi ya picha: