Michezo
Picha: Mashabiki wa Yanga wafika uwanjani alfajiri wakisubiri kuingia Uwanja wa Taifa
Klabu ya Yanga leo June 28 inaingia uwanjani katika mechi ya kombe la Shirikisho inawaalika klabu ya TP Mazembe kutoka DR Congo mchezo ambao utachezwa uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.
Mechi hiyo ambayo haina kiingilio ni bure tu kuingia uwanjani leo asubuhi mashabiki wanaoaminika kuwa ni wa Young Africans tayari wamejitokeza kwenye uwanja wa taifa jijini Dar es salaam wakisubiri muda wa kufunguliwa milango.
Mashabiki hao wapo tangu alfajiri wakisubiri kupewa utaratibu wa kuingia uwanjani kushuhudia mchezo huo.