Bongo5 ExclusivesPicha
Red Carpet Photos: LISA JENSEN ATWAA TAJI LA REDD’S MISS WORLD TANZANIA
Lisa Jensen amefanikiwa kutwaa Taji la Redd’s Miss Tanzania kwa mwaka 2012 baada ya kuwabwaga washiriki wenzake kumi.
Shindano hilo maalum kama Miss World Second Chance, lilihusisha washiriki wa mashindano ya Miss World waliopita ambao hawakufanikiwa kushinda taji hilo.
Kwa mujibu wa maelezo kutoka kampuni ya Lino International Agency,ambao ndio waratibu wa shindano hilo, Lisa ataenda kushindana warembo wengine nchini Mongolia katika shindano litakalo fanyika tarehe 29 mwezi huu.