Michezo
Picha: Lewis Hamilton anyakua ubingwa wa dunia wa mbio za magari za Formula One
Dereva wa Uingereza, Lewis Hamilton ameibuka mshindi wa mbio za magari wa dunia, Formula One – Abu Dhabi Grand Prix.
Hamilton akishangilia ushindi
“Hii ni siku kubwa zaidi katika maisha yangu,” alisema dereva huyo mwenye miaka 29 aliyeendesha gari ya Mercedes Benz.
Huo ni ushindi wa mara ya pili wa taji hilo baada ya mwaka 2008 na anaungana na madereva wengine wenye mataji mawili akiwemo Fernando Alonso.
Hamilton akipewa busu la ushindi na mpenzi wake,Nicole Scherzinger
Michael Schumacher anashikilia rekodi ya mataji mengi zaidi akiwa nayo saba. Mpenzi wake Nicole Scherzinger na familia yake walikuwepo kumshangalia.