BurudaniLady Jay Dee
Picha: Lady Jaydee ateuliwa kuwa balozi uzazi wa mpango
Msanii wa muziki nchini, Lady Jaydee ameteuliwa na hospitalI ya Marie Stops kuwa balozi wa kampeni ya Chagua Maisha inayohamasisha uzazi wa mpango na kupinga mimba za utotoni.
Akizungumza na TBC wakati ya kusaini mkataba wa hospital hiyo, Lady Jaydee amesema kampeni imempa nafasi ya kukutana na vijana kuwapa elimu kuhusu uzazi wa mpango. Lady Jaydee pia amesema anaweza kutoa ujumbe kwa kutoa nyimbo ambazo zitafikisha ujumbe kwa mwananchi kuhusu kuchagua jinsi kuishi kwa uzazi wa mpango.