Michezo
Picha: Kobe Bryant apewa heshima kubwa na jiji la Los Angeles
Mchezaji nguli wa kikapu nchini Marekani, Kobe Bryant amepewa heshima kubwa na jiji la Los Angeles ambapo Jumatano hii ilitajwa kama siku yake.
Tarehe hiyo ilikuwa ni mchanganyiko wa jezi alizozivaa kwenye career yake akiwa na Los Angeles Lakers, 8 na 24.
Alipewa alama ya jiji na meya wa Los Angeles, Eric Garcetti, akiwa na familia yake na wanasiasa wengine wa mji huo na kumtakia heri ya kuzaliwa, kwa kufikisha miaka 38, Jumatatu.
Kuonesha furaha kwa heshima aliyopewa, Kobe alitumia Twitter kuandika: ‘It was MY honour to play here for 20 years. Much respect, LA #Kobebryantday.’