Baada ya kuwa katika mahusiano yaliyodumu kwa miaka 7 na kufanikiwa kuweka uhusiano wao nje ya macho ya umma, msanii maarufu wa Bongo Kleyah amefunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu ambaye pia ni meneja mshirika, Mhandisi Barnabas Ndyanabo mjini Kampala, Uganda Septemba 10, 2016.
Harusi ilifanyika katika hoteli ya kifahari ya Serena. Sherehe hiyo ilibarikiwa na mualiko wa wageni 100 ambao ni watu wa karibu sana wa familia na marafiki.
Bongo songstress huyo alivalia lulu beaded fascinator na lace Berta vilivyonogesha gauni maalum lililotengenezwa na designer maarufu kutoka nchini Afrika Kusini na lilikuwa kama mermaid silhouette na alivalia viatu vya Bradgley Mischaka.
Barnabas alivalia Tuxedo maridadi. Mavazi haya yaliwafanya maharusi hawa kupendeza kupita maelezo .
Kleyah alisema, “Sisi tulitaka hii siku muhimu zaidi katika maisha yetu tusherehekee na watu wa karibu sana na familia na ndio mana tulialika watu 100 pekee na hatukutaka kufanya sherehe kubwa sana kwa sababu hii ni siku ya kuwa karibu na familia.”
Kleyah anasema daima ataendelea na maisha yake ya kimuziki hata baada ya kufunga pingu za maisha. Kleyah ni mtu ambaye kila siku hupendelea kuweka maisha yake binafsi na si mtu apendae kujulikana kwa maisha yake ya binafsi ukizingatia ndio kwanza ameanza muziki hivi karibuni. Amekuwa akipendelea kujulikana kwa mafanikio yake ya kimuziki na ndio maana amekaa mwezi mzima hadi kuja kutoa taarifa hii.
Wanandoa hao wenye furaha wamebarikiwa kuwa na binti mrembo wa miaka 4 aitwaye Eleanor. Baada ya ndoa amerejea kufanya muziki na pia ameahidi kufanya hits nyingi zaidi kwa kushirikiana na wanamuziki maarufu wanaojulikana ndani na nje ya Tanzania.
Amewataka wapenzi na mashabiki wake kujiandaa kupokea kazi zake mpya.
https://www.youtube.com/watch?v=-VlBY73LBMk