Msanii wa muziki wa Hip Hop, Kala Jeremiah anaendelea kufurahia maisha na mwanae kwa kupost picha katika mitandao ya kijamii ikiwa ni wiki mbili toka mpenzi wake ajifungue mtoto wa kiume aitwae ‘Alama’.
Rappa huyo aliimbaia Bongo5 hivi karibuni kuwa mtoto huyo anamchukilia kama zawadi maalum aliyopewa na Mungu katika maisha yake.
Kupitia ukurasa wake wa instagram, Kala ameandika:
Tangu nikufahamu sasa yapata wiki 3 umekuwa mtu mzuri sana kwangu. Umekuwa furaha ya kudumu moyoni mwangu. Ee Mwenyezi Mungu asante sana kwa kuniletea alama kwenye maisha yangu.