Picha: Joslin kuachia video yake mpya baada ya wiki mbili
Msanii wa kundi la Wakali Kwanza, Joslin aliyewahi kuhit na ngoma kama ‘Niite Basi’ anajipanga kuachia video ya wimbo wake mpya ambao ameshoot hivi karibuni.
Wimbo huo ameupa jina la ‘Only You’. Mara ya mwisho muimbaji huyo aliachia wimbo wake wa Tesa Naye mwezi Mei mwaka 2014 aliomshirikisha rapper Stopa Rhymes.
Kupitia mtandao wake wa Instagram, muimbaji huyo ameandika, “Yeah…the return of#Joslin…(ndoto yao)..” “Yeah…#Joslin you&i@charm_and_loyal_proya “ONLY YOU”..,” ameandika kwenye picha nyingine aliyoiweka kwenye mtandao huo.
Akiongea na Bongo5, muimbaji huyo amesema kuwa kwenye wimbo huo hakuna msanii aliyemshirikisha na video hiyo anatarajia kuiachia baada ya wiki mbili kama mipango yake ikienda sawa. Wakati huo huo Joslin amedai kuwa mipango yake ya kuzirudia nyimbo zake za zamani bado ipo pale pale kama alivyowahi kuahidi siku za nyuma.