Burudani
Picha: Jarida la Baabkubwa lazinduliwa upya Alhamisi hii
Alhamisi hii uongozi wa Baabkubwa umefanya sherehe ya uzinduzi wa jarida hilo katika ukumbi wa King Solomon ambalo limekosekana mtaani kwa kukaa kimya takribani kwa miaka miwili.
Bosi wa Baabkubwa akiwa na meneja wa jarida hilo
Sherehe hiyo ilihudhuriwa na watu kibao wakiwemo wasanii wa muziki, waigizaji, watayarishaji wa muziki, wabunifu wa mitindo, watangazaji na wadau wengine wa tasnia ya burudani hapa nchini. Lakini pia sherehe hiyo ilitumika kuwatambulisha viongozi wapya watakaolisimamia jarida hilo ambao wanaongozwa na mkurugenzi wa Candy and Candy, Joe Kariuki.
Tazama picha zaidi hapa chini za tukio hilo.