Burudani

Picha: Huyu ndio msanii wa Kenya aliyemshirikisha Diamond baada ya Victoria Kimani

Collabo ya mwisho ya Diamond Platnumz na msanii wa Kenya ni ile aliyoshirikishwa na Victoria Kimani kwenye wimbo Prokoto alikuwemo Ommy Dimpoz pia.

12042664_964200770314210_2861085196419878386_n
Akothee na Diamond wakiwa studio

Baada ya hapo, Diamond amekuwa akifanya ngoma na wasanii wa Nigeria, Afrika Kusini na Marekani zaidi. Hata collabo na wasanii wenzake wa Bongo zimekuwa za nadra pia na hivyo kumfanya kuendelea kuwa msanii anayetafutwa zaidi kwa collabo Afrika Mashariki.

Lakini kuna msanii wa Kenya aliyepata nafasi ya kumshirikisha staa huyo na huyo si mwingine zaidi ya Esther Akoth maarufu kwa jina la Akothee.

12042847_964200870314200_4474176626958980005_n
Akothee na Babu Tale

Muimbaji huyo amekuja nchini kurekodi wimbo huo na Diamond kwenye studio zake za Wasafi Classic, WCB. Wawili hao waliingia kwenye studio usiku wa kuamkia Alhamis hii.

12033189_964200813647539_5336874989264093516_n
Akothee akirekodi wimbo wake mpya aliomshirikisha Diamond

Hiyo inakuwa collabo ya pili kubwa kwa Akothee kuifanya mwaka huu baada ya hivi karibuni kurekodi wimbo na Flavour wa nchini Nigeria.

Hivi karibuni aliachia video ya wimbo wake ‘Shengerera Mama’ iliyoongozwa na God Father.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents