Picha: Hili ni gari la zaidi ya shilingi milioni 100 analoendesha Shetta
Ukitaja wasanii wa Tanzania wanaondesha magari ya kifahari zaidi basi usisahau kumweka Shetta kwenye orodha.
Mkali huyo wa Shikorobo anaendesha gari ambalo hutumiwa zaidi na mameneja au wafanyabiashara wakubwa – Land Rover Discovery, toleo jipya.
Gari analoendesha Shetta
Tumegoogle kuangalia bei ya magari hayo Afrika Kusini na tumebaini kuwa ukitaka kupata hata lililotumika tayari, basi jikusanye kuanzisha na Rand 400,000 – 800,000.
Inategemea amenunulia wapi lakini kwa madafu kupata gari kama hilo huna budi kuwa na mpunga unaoanzia shilingi milioni 100 na kuendelea!
Na kama unadhani kuwa kununua gari hilo kumejeruhi mifuko ya rapper huyo, basi umekosea. Alipost picha hiyo chini kwenye Instagram japo ikiwa na caption tofauti, ujumbe ulifika.
Muziki unalipa!