Picha: Hellen George aibuka mshindi wa Serengeti Super Nyota Diva 2014
Mwanadada Hellen George mkazi wa Sinza, Dar Es Salaam ameibuka mshindi wa Serengeti Super Nyota Diva 2014 baada ya kuwapiKu washindani wake 14 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania katika fainali hizo zilizofanyikia ndani ya ukumbi wa Escape 1 jijini Dar Es Salaam.
Mshindi wa Serengeti Super Nyota Diva 2014, Hellen George
Ushindi wa Hellen George utamfanya afanye kolabo na Diamond, kufanya nyimbo tatu ambazo zitasimamiwa kwa kila kitu pamoja na kupokea kitita cha pesa taslimu shilingi milioni moja kutoka kwa waandaaji wa tamasha la Serengeti Fiesta.
Pia Serengeti Super Nyota Diva kabla ya kufanya fainali iliwapa fursa vijana wa kike hao kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania kufundishwa taratibu mbalimbali za muziki kutoka kwa msanii Barnaba Elias.
Dj Fetty na Ditto, MMajaji wa fainali ya hiyo wakifuatilia tukio kwa umakini
Mshiriki wa Serengeti Super Nyota Diva kutoka Singida akisubiria uamuzi wa majaji
Mmoja kati ya washiriki wa shindano hilo