Burudani

Picha: Hawa ni washindi wa tuzo za EATV 2016, Alikiba akomba tuzo 3

Mwanamuziki Alikiba ndiye msanii aliyejishindia tuzo nyingi katika usiku wa Tuzo za EATV 2016 zilizofanyika Jumamosi hii katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es salaam.
img_9313
Alikiba akitoa neno la shukrani kwa mashabiki wake

Aidha msanii wa filamu Salim Ahmed aka Gabo Zigamba ameondoka tuzo mbili.

Wasanii ambao walifanya show usiku huo ni pamoja na Darassa, Billnass, Lady Jaydee, Barnaba, Vanessa Mdee, Shetta, Alikiba pamoja na Maurice Kirya.

List ya washindi wote wa EATV Award

1. Kipengele cha tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kiume 2016 kimekwenda kwa Ali Kiba.

2. Wimbo wa Aje wa Ali Kiba umeshinda tuzo ya Wimbo Bora wa Mwaka 2016.

3. Video ya wimbo wa Aje ya Ali Kiba imeshinda tuzo ya Video Bora ya Mwaka 2016.

4. Kipengele cha tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kike 2016 kimekwenda kwa Lady Jay Dee.

5. Tuzo ya Heshima inayotolewa kwa mtu/taasisi yenye mchango mkubwa katika sanaa ya Tanzania inakwenda kwa Dj Bonny Love.

6. Tuzo ya Filamu Bora ya Mwaka 2016 imekwenda kwa filamu ya Safari ya Gwalu ya Gabo Zigamba.

7. Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kiume 2016 inakwenda kwa mwigizaji Salim Ahmed maarufu Gabo Zigamba.

8. Tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike 2016 inakwenda kwa mwigizaji Chuchu Hans.

9. Navy Kenzo wameshinda tuzo ya Kundi Bora la Muziki 2016.

10. Mwanamuziki Man Fongo ameshinda tuzo ya Mwanamuziki Bora Chipukizi 2016.


Angalia picha za show pamoja na utoaji wa tuzo.

img_9175

img_9184

img_9220

img_9224

img_9237

img_9268

img_9275

img_9290

img_9295

img_9304

img_9307

img_9311

img_9313

img_9315

img_9321

img_9348

img_9352

img_9365

img_9366

img_9384

img_9405

img_9406

img_9414

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents