Burudani
Picha: Diamond alivyoungana tena na familia yake South
Diamond Platnumz ameungana tena na familia yake nchini Afrika Kusini.
Muimbaji huyo wa Nana aliyeenda nchini humo kwaajili ya maandalizi ya show ya BET Experience Africa, ametumia fursa hiyo kuonana tena na mchumba wake Zari The Bosslady na mwanae, Tiffah.
Kupitia Instagram, Diamond ameonesha picha akiwa na familia hiyo wakizunguka kwenye mitaa ya mji (ambao hakutaja ni upi).
“I always wanted to be a Good Daddy & Hubby!!!… #FamilyTime katoto kanapenda picha haka eti kanachungulia,” aliandika.
Zari pia ameshare picha nyingine inayomuonesha Diamond akiwa na stroller ya mtoto akimsukuma Tiffah.
“Out and about today,” ameandika.
Akaunti ya Tiffah nayo ipo busy kuonesha maisha yao. “After a long day with my dad…..,” wameandika.