Burudani
Picha: Davido a-share picha mpya za mtoto wake wa kike zinazomuonesha vizuri sura
Ukiachilia mbali Diamond Platnumz wa Tanzania na rapper AKA wa Afrika Kusini, Davido ni staa mwingine wa Afrika aliyepata mtoto hivi karibuni na anajivunia kuwa BABA.
Davido na mama wa mwanaye
Davido ambaye ni miezi mitatu imepita toka apate mtoto wa kike, amekuwa akishare na followers wake picha za mwanaye, ikiashiria kuwa ni jinsi gani uwepo wa mtoto huyo duniani unamuongezea furaha iliyoshindwa kukamilishwa na mali/mkwanja anaoumiliki kutokana na kazi yake ya muziki pamoja na utajiri wa wazazi wake.
Mtoto wa Davido
Wakati Diamond na Zari bado hawajataka kuionesha sura ya mtoto wao Tiffah, Davido ameshare picha mpya Instagram inayomuonesha vizuri sura ya mtoto wake. Picha hiyo ilisindikizwa na maneno: “GETTIN TOO BIG”.