Picha: BASATA imemuonea huruma Shilole kiaina?
Inaonekana simu tayari zimeshapigwa kwa baraza la sanaa la taifa BASATA kutoka watu wenye mamlaka ya juu zaidi katika kuhakikisha kuwa adhabu ya kufungiwa kujihusisha na muziki kwa mwaka mzima inapunguzwa ama inaondolewa kabisa.
Maswali yalianza kuulizwa baada ya Shilole kupost picha hiyo juu kwenye Instagram akitumbuiza kwenye moja ya kampeni za uchaguzi za CCM. Watu wengi walihoji kama BASATA limeondoa adhabu hiyo au amepewa msamaha katika kipindi hiki cha uchaguzi.
Muimbaji huyo pia wiki hii amesafiri hadi Texas, Marekani ambako yeye na Ommy Dimpoz watatuimbuiza.
BASATA lilimpa Shilole adhabu hiyo baada ya picha za aibu kusambaa mtandaoni zilizopigwa wakati akitumbuiza kwenye show ya nchini Ubelgiji.
Na sasa kwakuwa ameanza kufanya tena show huenda adhabu hiyo ikawa imeondolewa kimya kimya.