Miaka ya hivi karibuni mastaa kibao wametambua umuhimu wa kufanya mazoezi kujiweka vizuri kiafya na stamina.
Japo huko nyuma walianza kadhaa wakiwemo wakongwe kama P-Funk Majani, Diamond, Jux na wengine, huenda Mwana FA anaweza kuwa ni rapper aliyewavutia wasanii wengine kibao kuingia gym kutengeneza miili yao.
Ommy Dimpoz naye ameingia kwenye orodha hiyo ya wahudhuriaji wazuri wa gym.
Na sasa gym zimepata members wapya. Ni AY na Barnaba. Kama ulibahatika kukutana na AY hivi karibuni utagundua kuwa alikuwa amegain sana kiasi cha wengi kumshauri aanze kufanya mazoezi na sasa ameuzingatia na kuanzisha mkakati wa kuupunguza mwili wake.
Akipost picha akiwa kwenye gym, AY ameandika: Monday- Saturday #HitTheGymBeforeMasinema 90kgs –> 85kgs now heading to 75kgs Really Quick.. Blessings kwa @arnoldluciano & @ibra_carter.”
Naye Barnaba yupo kwenye mkakati kama huo na amekuwa akionesha safari yake mpya ya mazoezi kupitia Instagram.