Picha: Avril amrithi Vanessa kwenye show ya Ommy Dimpoz, Nakuru
Ommy Dimpoz alikuwa msanii pekee kutoka Tanzania aliyetumbuiza kwenye show ya ‘It’s Our Time to Part On’ iliyofanyika mjini Nakuru, Kenya kwenye mkesha wa mwaka mpya.
Ommy Dimpoz na Avril wakitumbuiza ‘Me And You’
Wasanii wa Kenya waliotumbuiza ni pamoja na Wyre, Avril, Jaguar, Juacali na Nameless.
Ommy Dimpoz alifanikiwa zaidi kuzikonga nyoyo za wapenda burudani wa Nakuru, pale alipomchukua Avril ambaye anatokea kwenye mji huo kutumbuiza hit single yake, Me and You aliyomshirikisha Vanessa Mdee.
Thank you Miss Avril ulitisha sana kwenye Me & U salute,” aliandika Ommy Dimpoz kwenye Instagram na mrembo huyo kujibu, “was such a pleasure sharing a stage with the incredible @ommydimpoz last night. #E.APamoja #MyCityMyTown #HappyNewYear!!.”
“@vanessamdee tried to represent you, I hope I did a good job,” aliongeza.
Tazama zaidi picha za show ya Ommy Dimpoz.