Picha: Anne Kansiime awasili Dar, tazama alivyopokelewa JNIA
Mchekeshaji Anne Kansiime amewasili Alhamis hii jijini Dar es Salaam tayari kwa burudani kali hapo August 2 kwenye ukumbi wa Golden Tulip. Mkali wa huyo wa kuchekesha na sanaa za majukwaani Afrika Mashariki, aliwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere majira ya saa kumi jioni kwa ndege ya shirika la Rwanda.
Anne Kansiime akisindikizwa na walinzi baada ya kuwasili
Anne anatarajiwa kuzungumza na waandishi wa habari hapo Ijumaa saa tano kamili asubuhi kwenye ukumbi wa Sports Lounge uliopo Posta, na Jumamosi atasalimiana na mashabiki katika viwanja vya Mlimani City. Burudani ya hiyo ya Anne, ambayo itasindikizwa na Fredi Omondi kutoka Kenya na Pilipili wa Tanzania, huku ikinogeshwa na bendi ya ODAMA, imeandaliwa na kituo cha Radio 5.
Tazama picha zaidi na mchekeshaji huyo akiwasili Dar.