Burudani
Picha: Akothee aonesha jeuri ya fedha, amkabidhi mwanae zawadi ya gari kwenye birthday yake
Akothee sio mtu wa mchezo mchezo. Mrembo huyo wa Kenya ameonesha jeuri ya fedha kwa kumzawadia mwanae gari la kampuni ya Mazda katika sherehe yake ya kuzaliwa ya kutimiza miaka 19 wikiendi hii.
Mtoto huyo ambaye kwenye mtandao wa Instagram anatumia jina la @Baby Rue alimshukuru mama yake kwa kuandika, “The moment I saw this walking in i was too shocked to speak…mummy u wil always remain the best mother in the world@akotheekenya ….i love my new toy and yes i wunt accept any lift coz i got myn.. thank yu mummy????????????????????.”
Sherehe hiyo ilifanyika katika hoteli ya Villa Rosa Kempinski iliyopo Nairobi, Kenya. Tazama picha zaidi za sherehe hiyo hapa chini.