BurudaniVideos

Petit Money aelezea uhusiano wake ulivyo sasa na shemeji yake Diamond na bosi wake Wema Sepetu (Video)

Ahmed Hashim Ngahemela kama anavyojulikana zaidi kwa jina la Petit Money anafahamika zaidi kwa kuwa mmoja wa waliokuwa wafanyakazi wa Wema Sepetu na pia aliyekuwa mume wa dada yake na Diamond, Esma.

13167220_1602429520073423_920288138_n

umezungumza naye kutaka kufahamu uhusiano wake na shemeji yake Diamond ukoje licha ya kuwa upande wa Wema ambaye haziivi tena na Diamond.

“Mitihani inakuwa mingi, ni lazima itokee lakini watoto wa kiume mitihani tumeumbiwa sisi. Mitihani mingi sana imetokea, wakati mgumu sana umetokea baina ya timu zile mbili kuwa tofauti na mimi ndio nimebase sehemu zote, huku na huku lakini nashukuru niliplay part yangu vizuri,” amesema Petit.

“Mimi sina tatizo na Diamond, ni shemeji yangu na ni family sababu mimi nilishazaa na dada yake hata kama ikawaje siwezi nikawa na tatizo naye, tukikutana njiani tunasalimiana, mimi ninadili ntampigia, hatuna tatizo.”

Kwa sasa Petit ni meneja wa Billnass na Nuh Mziwanda, kitu ambacho anasema kimesababisha maelewano hafifu na bosi wake wa zamani, Wema Sepetu.

“Mimi sidhani kama nina tatizo na Wema. Ndiye aliyenifanya mimi nijulikane na Wema ndiye mtu ambaye mimi nimetoka naye mbali sana miaka tisa. Kwahiyo hata kama nikiwa nimegombana naye siwezi nikasema siongei naye, kwahiyo mimi nahesabia sina tatizo naye kama watu wanavyodhani,” ameongeza.

Tazama zaidi interview hapo juu.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents