Michezo
Peter Cech ashinda tuzo moja kwa mara ya 9
Golikipa namba moja wa klabu ya Arsenal, Peter Cech ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa Jamhuri ya Czech kwa mwaka 2016. Hii ni mara 9 mchezaji huyo anashinda hiyo tuzo.
Cech ambaye saivi anamiaka 34, ameshastaafu kuichezea timu ya taifa ya Jamhuri ya Czech tangia mwaka jana baada ya michuano ya Euro nchini Ufaransa, amestaafu akiwa ameichezea timu hiyo mechi 124.