Pambano la Tyson na Klitschko laahirishwa tena
Mpiganaji masumbwi ambaye ni bingwa wa uzani mzito kutoka Uingereza Tyson Fury ameahirisha tena pambano lake la marudiano dhidi ya Wladimir Klitschko kwa mara ya pili kwasababu ”afya yake hairidhishi”.
Mapromota wake hawakueleza undani wa taarifa zaidi lakini wamesema ” hali yake ni mbaya mno na haimruhusu kushiriki pambano hilo”.
Fury, mwenye umri wa miaka 28, alimshinda Klitschko kutoka Ukraine kwa pointi katika pambano la kwanza mnamo Novemba mwaka jana.
Marudio ya pambano la awali lilipangwa Julai 9 katika uwanja wa Manchester Arena, na liliahirishwa hadi Juni baada ya Fury kuvunja fupa la kisigino chake.
Pambano jipya la marudio kati ya mabondia hao wawili lilipangwa kufanyika Octoba 29.
“Tyson sasa inabidi afanyiwe matibabu anayohitaji ili aweze kupona kikamilifu,” Hennessey Sports iliongeza.
“Tunaomba radhi kwa wote wanaohusika katika pambano hili na mashabiki wote wa masumbwi waliotazamia maruduo hayo. Ni wazi kuwa Tyson pia amehuzunishwa na hali ilivyo.
“Tutatoa taarifa zaidi katika muda unaofaa.”